VICHWA VYA HABARI

Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks t>

Sunday, April 24, 2016

Tishio la usalama linalokabili eneo la mpaka wa Kenya na Somalia sasa Bomba la mafuta la Uganda litapitia Tanzania

Kator fm (File)
Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wametangaza kuwa bomba la mafuta la Uganda kutoka Hoima hadi Bandari ya Tanga litapitia Tanzania, mradi ambao unatarajiwa kugharimu dola za kimarekani bilioni 4.
Viongozi hao wamefanya uamuzi huo kwenye Mkutano Mkuu wa 13 wa Ushoroba wa Kaskazini uliomalizika mjini Kampala, ambao pia umeamua kuwa bomba jingine la mafuta litajengwa nchini Kenya kutoka eneo la Lokichar hadi bandari ya Lamu.
Vyombo vya habari vya Uganda vimeona kuwa, uamuzi wa kujenga bomba hilo kupitia Tanzania unatokana na tishio la usalama linalokabili eneo la mpaka wa Kenya na Somalia.
http://swahili.cri.cn/141/2016/04/25/1s152805.htm 

Nguli wa muziki wa Rhumba, Papa Wemba afariki dunia

Jules Shungu Wembadio Pene Kikumba, anaejulikana kwa jina maarufu Papa Wemba, ameiaga dunia akiwa katika jukwaa Jumapili Aprili 24. Mwanamuziki huyu nguli wa Congo (DRC) alikuwa na udhaifu wakati wa tamasha aliloendesha nchini Cote d'Ivoire Jumamosi Aprili 23.http://www.kiswahili.rfi.fr/utamaduni/20160424-gwiji-wa-muziki-wa-kiafrika-papa-wemba-afariki
Papa Wemba, mwimbaji na mtunzi wa Muziki wa Afrika.
© E. Sadaka
 Msemaji wa serikali, Lambert Mende imeelezea huzuni ilio nao kwa kumpoteza msanii


mkuu Papa Wemba, mfalme wa muziki wa Rumba.
Nyota wa soka wa Cameroon, Samuel Eto'o, ameelezea kuwa ana huzuni mkubwa kuona amemkosa gwiji wa muziki wa Kiafrika.
Waandaaji wa tamasha la miziki ya miji ya Anoumabo (FEMUA), ndio wametangaza kifo chake Jumapili asubuhi. Papa Wemba alikuwa na umri wa miaka 66. Raia wa Afrika ya Kati na kungineko wamejawa na huzuni na hisia.


Papa Wemba alikua na udhaifu wakati wa tamasha alilopiga mjini Abidjan, Jumamosi, Aprili 23, katika tamasha la FEMUA 2016, ikiwa ni tamasha la miziki ya miji ya Anoumabo. Amefariki alipofikishwa hospitalini Jumapili asubuhi, baada ya kuanguka ghafla akiwa jukwaani. Kifo chake kimetangazwa saa sita mchana na waandaaji wa FEMUA.
Udhaifu kwenye jukwaa
Hisia kubwa na huzuni mjini Abidjan Jumapili hii, mwandishi wetu, Olivier Rogez, amearifu. Mwanamuziki, ambaye alikua akihitimisha tamasha hilo, alikuwa kwenye jukwaa saa 11:00 alfajiri. Kulikua na joto kubwa na Papa Wemba alikua na ishara ya uchovu. Aliomba mara kadhaa kuongeza sauti ya vipaza sauti. Mwanamuziki huyo nguli wa Congo alianguka alipokua akiimba mwimbo wa nne.
Papa Wemba aliondolewa kwenye jukwaa baada ya kupoteza fahamu. aliondolewa sehemu hiyo na timu za waokoaji, Olivier Rogez amearifu, na kusafirishwa katika hospital ya karibu lakini mwanamuziki huyo hakuwa na muda tena wa kuishi duniani. "Wakati nitakua bado na uwezo wa kuimba, nitaimba," alisema Papa Wemba siku chache kabla ya kifo hicho kumkuta, ametoa ushuhuda Claudy Siar akiwa mjini Abidjan, ambako pia anahudhuria tamasha la FEMUA kwa niaba ya RFI.
Mwanamuziki nguli wa muziki wa Rumba
Papa Wemba alizaliwa mwezi Juni 1949 katika jimbo la Kasai-Masharikil (DRC), na alikua gwiji wa muziki wa Kiafrika. Katika miaka ya 1950, muziki wa Rumba kutoka Congo ulitawala barani Afrika na bado unatikisa na kuchezwa jukwaa mbalimbali barani la Afrika. Papa Wemba pamoja na bendi ya Zaiko Langa Langa waliinua Rumba kwa kiasi fulani na kweza kuchezwa katika jukwa za kimataifa.
Wasifu wa Papa Wemba
Papa Wemba alikuwa mwanzilishi wa studio na bendi ya Viva la Musica mwaka 1977, na alicheza nyimbo kama vile Analengo mwaka 1980, na baadaye Maria Valencia au Yolele, nguli wa "muziki wa dunia". Ni kwa msaada wa mwanamuziki wa Uingereza Peter Gabriel ndiye alimfanya Papa Wemba kujulikana duniani.
Papa Wemba aligundua na aliweza kuvipa mafunzo vizazi vya wanamuziki wa Afrika kama Koffi Olomide.
Papa Wemba alishiriki katika vipindi vingi vinavyorushwa hewani na RFI.
http://www.kiswahili.rfi.fr/utamaduni/20160424-gwiji-wa-muziki-wa-kiafrika-papa-wemba-afariki

 

Friday, April 22, 2016

Uganda mwenyeji wa mkutano kuhusu miundombinu


ICGLR, Kampala, Agosti 7, 2012.
REUTERS/Edward Echwalu

    
 
Marais wa Kenya, Uganda, Rwanda na Sudan Kusini wanatarajiwa kukutana kesho jijini Kampala nchini Uganda katika kikao cha 13 kujadili kuhusu maendeleo ya miundo mbinu zinazounganisha nchi hizo nne.







Miongoni mwa miradi ambayo mataifa hayo yanashirikiana ni pamojana ujenzi wa reli ya Kati na ujenzi wa bomba la kusafiria mafuta.
Inaelezwa kuwa, Uganda inatarajiwa kufafanulia Kenya kwenye kikao hicho ni kwanini umeamua kujenga bomba lake la kusafirishia kupitia bandari ya Tanga.
Hayo yakijiri, viongozi wa Kenya, Uganda na Tanzania mwishoni mwa wiki wanatarajiwa kutoa uamuzi wa mwisho kuhusu ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Uganda na Kenya hadi pwani.
Mwaka jana, Kenya na Uganda zilikuwa zinashauriana kuhusu mpango wa kujenga bomba la kusafirisha mafuta kutoka Hoima, magharibi mwa Uganda, hadi bandari ya Lamu katika Pwani ya Kenya.
Bomba hilo la mafuta lilikusudiwa kutumiwa kusafirisha mafuta ghafi kutoka eneo la Ziwa Albert nchini Uganda na kutoka eneo lenye mafuta la Lokichar nchini Kenya.
http://www.kiswahili.rfi.fr/eac/20160422-uganda-mwenyeji-wa-mkutano-kuhusu-miundombinu


Serikali ya Tanzania ndio mmiliki wa kampuni ya General Tyres Arusha


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, wa Tanzania Bw Charles Mwijage amesema hivi sasa kiwanda cha kutengeneza matairi cha General Tyre Arusha kinamilikiwa na serikali baada ya serikali kununua asimilia 26 kutoka kwa mbia wake. Akizungumza bungeni, Bw Mwijage amesema serikali imeweka dhamana ya kusimamia na kuendesha kiwanda hicho, chini ya shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) na kwamba tangazo la Serikali (GN) kuhusu uamuzi huo litatolewa wakati wowote kuanzia sasa. Amesema dhamira ya serikali ni kuona kiwanda hicho kinaanza kuzalisha matairi mapema iwezekanavyo. Pia shirika hilo litatoa majibu ya kiufundi na kijamii na kwamba ni lazima lizingatie maoni ya wadau wa sekta husika kwa ajili ya kuboresha kiwanda hicho. Aidha, mradi huo utaendeshwa chini ya menejimenti ya rasilimali watu wenye weledi katika biashara ya matairi na bila kutegemea ruzuku kutoka serikalini. Awali kiwanda hicho kiliacha uzalishaji mwaka 2009 baada ya serikali kukosa fedha za kukiendesha huku mbia mwenza kampuni ya Continental AG, kutokuwa tayari kuendelea na uwekezaji huo.
 http://swahili.cri.cn/141/2016/04/22/1s152770.htm

Ukuaji wa sekta ya viwanda bado uko nyuma Tanzania


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya bajeti nchini Tanzania imesema ukuaji wa sekta ya viwanda katika awamu ya kwanza ya mpango wa maendeleo ya taifa ulikuwa chini ya lengo, jambo ambalo haliridhishi maendeleo ya uchumi wa viwanda.
Akizungumza na radio China kimataifa, mwenyekiti wa kamati hiyo Hawa Ghasia amesema ukuaji wa sekta ya viwanda katika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mpango huo ulikuwa asilimia 6.6 chini ya lengo la kufikia wastani wa asilimia 11 mwaka 2015.
Amesema jambo hilo haliridhishi maendeleo ya uchumi wa viwanda na kusisitiza kuwa sekta ya madini katika utekelezaji wa mpango wa awamu ya kwanza haukuwa na mabadiliko makubwa kwenye Pato la Taifa kwa mwaka 2010. Kwa upande wake, naibu msemaji wa upinzani bungeni wa wizara ya fedha na Mipango Bw David Silinde amelitaka bunge kupitisha azimio ili kamati ya bunge kuhusu bajeti iwasilishe muswada wa sheria ya kusimamia utekelezaji wa mpango huo.

http://swahili.cri.cn/141/2016/04/22/1s152771.htm 

Tanzania kuanza kutekeleza ahadi ya Magufuli

Serikali ya Tanzania imesema itaanza kutekeleza ahadi ya rais John Magufuli ya kukipa kila kijiji nchini Shilingi milioni 50 katika mwaka wa fedha wa 2016-2017.
file katoro fm
Akizungumza bungeni, naibu waziri ofisi ya rais, Bw Antony Mavunde amesema utaratibu wa kugawa fedha hizo unaandaliwa na baraza la uwezeshaji wananchi kwa kushirikiana na wizara ya Utawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.Ameongeza kuwa vigezo ambavyo vimekuwa vikitumika katika kutoa mikopo na mitaji kwa vijana ni umri usiozidi miaka 35 ambapo vijana watahitajika kujiunga na Saccos za wilaya na kuunda vikundi na kuvisajili kisheria.Amesema ili kuhakikisha vijana wanakuwa wajasiriamali na wanaweza kupatiwa mikopo na mitaji, serikali imejiwekea mikakati ya kutambua vijana na mahitji yao katika ngazi mbalimbali na kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa makundi mbalimbali ya vijana.
http://swahili.cri.cn/141/2016/04/22/1s152772.htm 

Wednesday, April 20, 2016

Wafanyabiashara 13 kutoka nchini Oman wawasili mkoani Mtwara nchini Tanzania kuangalia fursa za uwekezaji

Picha File Katoro Fm
Wafanyabiashara 13 kutoka nchini Oman wamewasili mkoani Mtwara nchini Tanzania kuangalia fursa za uwekezaji na jinsi watakavyoshirikiana na Watanzania katika masuala ya kiuchumi.
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego alisema mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa kuwasili kwa wawekezaji hao ni fursa ya pekee kwa mkoa huo.
Alisema wafanyabiashara hao wamelenga kuwekeza katika maeneo mbalimbali ikiwamo sekta za kilimo, utalii, gesi na mafuta.
Kaimu Meneja wa Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asili Madimba, Mhandisi Nkilila Lucas alisema wafanyabiashara hao wana jukumu la kuwekeza katika sekta ya mafuta na gesi.
Mfanyabiashara kutoka Oman, Mansul Hemed alisema ziara hiyo imelenga kuangalia shughuli za uwekezaji na jinsi watakavyoweza kutoa elimu.
Alisema wafanyabiashara wa Kitanzania kwa sasa wanaweza kupeleka bidhaa zao Oman kama vile mifugo na mazao yanayolimwa nchini.
Wafanyabiashara hao wamewasili nchini na kutembelea maeneo mbalimbali yenye fursa za kiuchumi
http://swahili.cri.cn/141/2016/04/20/1s152718.htm